MAJALIWA: VIJANA JIWEKEENI MALENGO YA KULISAIDIA TAIFA

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka vijana wa Kitanzania wahakikishe wanajiwekea malengo ya kusoma kwa bidii ili kupata maarifa yatakayolisaidia Taifa kupata maendeleo. Pia, Waziri Mkuu amesema kuwa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ameiagiza Wizara ya Elimu kufanya mapitio ya sera ili kuifanya sekta hiyo kuendelea kufanya vizuri zaidi Ameyasema hayo leo (Jumatatu, Januari 24, 2022)